Wednesday, March 14, 2012

Umuhimu wa Omega 3 Kwa mama Mjamzito


Omega 3 humsaidia mtoto kukuza ubongo, kutengeneza retina kwenye mboni ya macho, na kutengeneza nervous system.

Omega 3 humsaidia mama kuzuia preeclampsia na postpartum depression. 

Njia kuu mtoto kupata Omega 3 ni kutokana na vyakula anavyokula mama. Kama mama atashindwa kupata vyakula vya kutosha vyenye Omega 3 basi mtoto atachukua Omega 3 iliyoko mwilini mwa mama ambayo mara nyingi iko kwenye ubongo wa mama. 

Basi iwapo mama hatapata Omega 3 ya kutosha anaongeza risk ya kupata Pospartum depression, mtoto mwenye uzito mdogo, preterm labor(mtoto kuzaliwa kabla ya muda), au csection(kuzaa kwa upasuaji).

Watoto ambao wamepata Omega 3 ya kutosha wameonyesha kuwa na attention spans kubwa na upeo mzuri kuliko watoto wengine. Pia walikuwa mbele zaidi katika ukuaji.

Kwa watoto hupunguza matatizo ya kitabia, na kwa watu wazima hupunguza chance za kupata kansa ya maziwa na prostate.

Hata kama wewe si mjamzito ni vizuri kupata Omega 3 ya kutosha kupitia mlo wa kila siku. 

Wakati wa ujauzito unashauriwa kupata angalau 250mg kila siku na katika trimester ya mwisho( miezi mitatu ya mwisho) kwasababu katika kipindi hiki mtoto hutumia asilimia 70 ya Omega 3 kujenga ubongo wake na nervous system yake.

Vyanzo vya Omega 3 katika Vyakula:

Omega 3 inapatikana katika samaki na mafuta ya samaki hasa hasa samaki wenye mafuta mengi kama vibua(mackerel), herring, salmon, dagaa, tuna.

Vyakula Vyenye Omega 3


Lakini ni vizuri pia kujua kwamba samaki wengi siku hizi wamekuwa na sumu ya mercury kwasababu ya machafuko ya kimizingira hivyo unaweza pia ukapata Omega 3 kutoka kwenye mayai, mkate, juice, mboga za majani, canola, sunglower, flaxeed oils na walnuts.

Na kama utapenda kunywa vidonge vya Omega 3 uhakikishe kwamba havijatengenezwa na maini ya samaki kwani hizi zina asilimia kubwa ya retinol Vitamin A, ambayo imegundulika kusababisha madhara kwa watoto. 

Omega 3 iliyotengenezwa kutoka kwa nyama ya samaki na sio maini ni bora zaidi. Kama huna uhakika ni bora kununa vidonge maalum vya Omega 3 vilivyotengenezwa kwa ajili ya wamama wajawazito.

3 comments:

  1. Je, Ni aina gani ya samaki ambao wana madini ya zebaki? Mama mjamzito anatakiwa ale samaki wapi ili asipate madhara?

    ReplyDelete
  2. Nikiwa mjamzito naweza kufunga kula chakula masaa 24?

    ReplyDelete