Thursday, May 24, 2012

Kuvimba kwa viungo vya mwili wakati wa ujauzito (water retention)


Wakati wa ujauzito mwili hutengeneza asilimia 50 zaidi ya damu na maji maji ili kumtosheleza mama na mtoto. Kuvimba kwa mwili wa mama ni kitu cha kawaida kwa ajili ya kuongezeka kwa damu mwilini. Na kuongezeka kwa pressure kwenye mishipa ya miguu na mikono kwa ajili ya ukuaji wa mtoto. Mama huweza kuvimba usoni, mikono, miguu.

Kuongezeka kwa maji mwili pia husaidia kulainisha mwili ili kusaidia kuongezeka kwa mwili mtoto anavyozidi kukua, pia husaidia kufungua misuli ya hips na chini ya tumbo ili kutayarisha njia ili mtoto aweze kupita.
Kuvimba kunaweza kutokea wakati wowote wa ujauzito lakini mara nyingi hutokea kuanzia mwezi wa tano 


Kuvimba pia kunaweza kusababishwa na:

Joto.

Kusimama kwa kipindi kirefu.

Kazi nyingi katika siku yako.

Diet yako ikiwa haina potassium ya kutosha.

Kunywa kahawa au vyakula na vinywaji vyenye kahawa kwa wingi.

Diet yako ikiwa na sodium au chumvi nyingi.

Kuvimba kunaweza kupunguzwa kwa 


Kula vyukula vyenye potassium kwa wingi kama ndizi na  hasa hasa tunda la cantaloupe.

tunda aina ya cantaloupe


Usisimame kwa kipindi kirefu.

Usikae nje kwa muda mrefu hasa wakati wa joto.

Ukipumzika elekeza au egemeza miguu juu.

Vaa viatu ambavyo viko comfortable na usivae viatu virefu.

Usivae nguo za kubana hasa hasa kwenye maeneo ya mikono na miguu.

Pumzika vya kutosha.

Pata zoezi la kuogelea.

Pata mazoezi kila siku lakini usipitilize

Unaweza kujikanda kwenye sehemu zilizovimba.

Kunywa maji kwa wingi hii itasaidia kutoa maji mwilini na kupunguza uvimbe. Na jaribu juice natural organic za cranberry na dhabibu. Nikisema natural au organiz na maanisha zile zilizotengenezwa na matunda asilia na hazijawekwa sukari ya kuongezwa au makemikali.

juice ya dhabibu
juice ya cranberry
juice na matunda ya cranberry



Punguza chumvi kwenye vyakula na diet yako kwa ujumla.

Ongeza Protein katika diet yako.

Kumbuka wakati mwingine kuvimba ni tatizo la kawaida na huashiria kuwa ujauzito unaendelea vizuri.

Mwombe mpenzi mumeo au mtu wa karibu nyumbani akupe massage ya maeneo yaliyovimba na mafuta. Hasa hasa mafuta ya grapeseed(mafuta ya dhabibu) yanaweza kusaidia.

mafuta ya dhabibu

Zamisha miguu kwenye maji yenye mafuta ya cypress hii husaidia mzunguko wa damu au mafuta ya lavender na chamomile hizi husaidia kurelax.

mafuta ya cypress

mafuta ya chamomile
mafuta ya lavender

Kuweka majani cabbage kwenye sehemu iliyovimba itasaidia kutoa maji na kupunguza maumivu.

  • Weka cabbage kwenye fridge sio freezer halafu yafute na kitambaa lakini usiyasafishe .
  • Weka vipande hivyo kwenye sehemu zilizovimba halafu ziache hapo mpaka zilowe halafu rudia na majani mengine fresh mpaka maumivu yapungue.Unaweza kufanya hivi mara nyingi mpaka pale unapopata nafuu.

No comments:

Post a Comment