Monday, March 12, 2012

Kiungulia na Gas wakati wa Ujauzito

Kila ujauzito uko tofauti lakini kuna baadhi ya vitu ambavyo wanawake wengi huwa wanaexperience katika ujauzito wao hivi ni pamoja na kiungulia(Heartburn) na kusikia gesi tumboni. Leo tutaongelea jinsi ya kuepukana au kuponya vitu hivi ukiwa katika hali hii. Katika nakala zijazo tutajaribu kugusia matatizo mengine ambayo yako common kwa wamama wajawazito.



Kiungulia(Heartburn)

Inaweza kusababishwa na nervous tension, hali ya acidi nyingi katika tumbo,kurelax kwa misuli ya tumbo ambayo itasababisha chakula kurudi juu tumboni, au kwa sababu ya ukuaji wa uterus basi tumbo limesukumwa juu. Hii hali inawakumba wanawake wengi katika nusu ya mwisho wa ujauzito

1. Jaribu kuchunguza ni vyakula gani ukishakula unapatwa na kiungulia. Ukisha vitambua viondoe katika diet yako ya kila siku. Mara nyingi vyakula vyenye mafuta au vyakula vyenye spices nyingi ni tatizo kwa wanawake wengi.

2. Jaribu kufanya mazoezi kidogo ukipatwa na hali hii.

3. Kula mapapai,mananasi, apples au mtindi, maziwa pia mkate uliokaushwa(toast) baada ya mlo. Hivi vyakula vinaweza kusaidia kutuliza kiungulia.

4. Wakati wa kula, jaribu kula chakula katika portion ndogo ndogo badala ya kula mlo mmoja mkubwa kamili. Pia jaribu kula taratibu na tafuna chakula vizuri.

5. Usinywe vinywaji vyenye gas.

6. Jaribu kutembea baada ya mlo.

7.Kula milo midogo mingi mfano kama uko mbali na nyumbani kula karanga au matunda yaliyokaushwa .

8.Usinywe vinywaji wakati wa kula, jaribu kunywa maji mengi kabla au baada ya mlo. Kama lazima unywe wakati wa kula basi kunywa glas ya maji yenye nusu ndimu iliyokamuliwa.

9. Kahawa na sigara zinachangia kwa kuudhi tumbo.

10. Usiwe unalala mara baada ya kula.

11. Chai aina ya "Anise" au "Fennel" baada ya mlo inasaidia tumbo kufanya kazi ya kusaga chakula vizuri.


Matatizo ya Gas

1. Jaribu kuchunguza ni vyakula gani ukishakula vinasababisha gas. Ukisha vitambua viondoe katika diet yako ya kila siku.

2. Lala na jaribu kuvuta pumzi kutoka tumboni.

3. Fanya zoezi la Pelvic Rocking(Zoezi la tatu katika nakala hii "Mazoezi maalum kwa mama mjamzito").

4. Usinywe vinywaji vyenye gas.

Umuhimu wa Folic Acid Kwa Mama Mjamzito

Folic Acid ni jamii ya Vitamin B inayosaidia katika ukuaji na utengenezaji wa cell za mwili ambazo ni muhimu sana katika wiki za mwanzo za ukuaji wa mtoto. 

Inasaidia katika kutengeneza ubongo na uti wa mgongo. Bila ukuaji mzuri wa hivi viungo kuna chance kubwa zaidi ya kupoteza mtoto kwa miscarriage na pia wanaweza wakapata matatizo ya nerve(Neural Tube Disorder)

Haya matatizo yanaweza kujitokeza kama magonjwa ya spina bifida na nancephaly. Matokeo yake ni kwamba mtoto anaweza akaparalzye miguu na kupata magonjwa ya kibofu na haja.

Magonjwa kwa mtoto aliyekosa Folic Acid Ya Kutosha

Umuhimu wa Folic Acid:
  • Utengenezaji mzuri wa cell za mwili.
  • Utengenezaji mzuri wa damu.
  • Kupunguza risk za magonjwa ya moyo na stroke.
  • Husaidia kukinga magonjwa kama cancer, colon cancer na cervical cancer.
  • Hupunguza chance ya kupata magonjwa ya Alzheimers.

Vyakula vyenye Folic Acid:

Mboga nyingi za majani ni vyakula vizuri vyenye Folic Acid, majani ya kunde, maharage, kuku, nyama ya ngombe, uyoga, spinach, lettuce, broccoli, mahindi, maparachichi na juisi ya machungwa, juisi ya nyanya.
Vyakula Vyenye Asilimia kubwa ya Folic Acid


Wednesday, March 7, 2012

Umuhimu wa Calcium na Magnesium kwa mama Mjamzito na anayenyonyesha


Mama mjamzito au anayenyonyesha anahitaji 1600 hadi 2000 mg za calcium kila siku. Kwa sababu wanawake wengi hawali vyakula bora huwa wanaishia kupata 600mg kwa siku ambazo hazitoshi. Calcium ni muhimu sana kwa mama na mtoto wakati wa ujauzito na kunyonyesha. 



Kwa mama calcium inasaidia kuweka blood pressue sawa na kupunguza kupata magonjwa kama preeclampsia ugonjwa unaoweza kumpata katika miezi ya mwisho ya ujauzito. Calcium pia inamsaidia mama kuweza kupata usingizi mzuri usiku na kupunguza kuuma kwa miguu. Hivyo ni vizuri kupata chakula chenye calcium kabla ya kulala.

Kwa mtoto afya njema inapatikana pale anapopata mg 200 hadi 300 ya calcium kwenye skeleton yake wakati wa trimester ya tatu. Pia kiwango hicho kinapatikana kutoka kwenye maziwa ya mama pale atakapozaliwa na kunyonya. Mama akipata kiwango kinachotakiwa cha calcium itamsaidia mtoto kusawazisha blood pressure yake pindi atakapozaliwa.

Mwili wa mama mjamzito unauwezo zaidi wa kuweka calcium kwenye mifupa  na mwili kuliko mwanamke asie mjamzito. Hii ni njia ambayo inamsaidia mwanamke mjamzito kuhimili mahitaji ya mtoto katika trimester ya tatu na baada ya kujifungua anaponyonyesha. Kama mama ataweza kupata calcium nyingi wakati wa ujauzito basi hata baadaye akizeeka anaweza kujikinga na magonjwa ya osteoporosis(kulainika kwa mifupa) ambayo hutokea katika miaka hiyo.

Magnesium
Magnesium na Calcium inasaidiana kwa kiasi kikubwa katika kuendesha shughuli mbali mbali za mwili. Kukosekana kwa Magnesium ya kutosha wakati wa ujauzito kunaweza kusababisha kupata uchungu kabla ya muda, na kuongezeka kwa matatizo ya nerve kwa mtoto kama ya cerebral palsy.

Vyakula vyenye Calcium


Maziwa na vyakula vyenye jamii ya maziwa kama jibini na mitindi vina Calcium nyingi za kutosha. Vyakula vingine ni pamoja ufuta, tuna, kale, mustard greens, maharage, mayai, spinach na whole grains.




Vyakula vyenye Magnesium
Mboga za majani yenye rangi za kijani iliyokolea, whole grains, vyakula jamii ya karanga na njegere. Pia kula vyakula na juisi ya machungwa itakupa vitamin c ambayo itawezesha mwili kutumia Calcium, Iron na folic acid kwa ufanisi zaidi. 



Kuliko kutumia vitamin supplement za calcium na magnesium ni vizuri mama akijitahidi kupata hivi virutubisho moja kwa moja kutoka kwenye chakula kwani baadihi ya madawa yanauwezo kusababisha lead poisoning kama zikitumiwa kwa muda mrefu.

Mama kupata magnesium ya kutosha kutamsaidia mtoto wakati wa labor. Mdundo wa moyo wa mtoto wakati wa labor unakuwa uko sawa na pia kuzuia matatizo mengine kwa mtoto wakati wa labor.

Kwa mama magnesium ya kutosha kutamkinga na ugonjwa ya preeclampsia(high blood pressure wakati wa trimester ya mwisho wa uzazi na kuwa na protein nyingi katika mkojo kwasababu mwili unashindwa kuutumia ipasavyo) na kupatwa na uchungu kabla ya wakati unaotakiwa.

Tuesday, March 6, 2012

Ratiba ya mazoezi kwa mama mjamzito Wiki ya Kwanza


Kwa wale mlioniuliza jinsi ya kupangilia haya mazoezi katika siku yako, nawapa ratiba ya mazoezi kwa maelezo zaidi ya kila zoezi angalia katika maada zilizopita. 

Maelezo ya jinsi ya kuyafanya haya mazoezi na umuhimu wake:


Hii ratiba ni kwa wale mnaoanza kwa mara ya kwanza nitawapa ratiba nyingine wiki ijayo kuongeza challenge kidogo katika mazoezi.

Mazoezi kwa mama Mjamzito Wiki ya Kwanza:


Monday, March 5, 2012

Mlo Bora Kwa Mama Mjamzito Sehemu Ya Kwanza


Kwa ajili ya afya ya mama na mtoto ni muhimu sana mwanamke apate chakula bora. Ukosekanaji wa chakula bora kunaweza kukasababisha mtoto kuzaliwa kabla ya mda wake au na uzito mdogo ambao unaweza ukachangia katika kuzuia ukuaji wa ubongo na mwili. 

Kwa mama anaweza akapata anaemia, infection, matatizo katika placenta, matatizo katika labor, c-section(kuzaa kwa upasuaji wakati wa kujifungua), kutokupona kwa haraka, matatizo katika kunyonyesha, toxemia na pre-eclempisa(haya ni magonjwa yanayosababishwa na maini kutoweza kufanya kazi yake vizuri na mwili kujitahidi kutoa protein kutoka sehemu nyingine za mwili kwa sababu hamna protein ya kutosha). 

Dalili zake ni pamoja na kuwa na protein kwenye mkojo, blood pressure kuwa juu, kuumwa kwa kichwa, kusikia kizungu zungu, kuzimia, kuvimba kwa viungo n.k


Mama mjamzito anatakiwa apate 100 grams za protein kwa siku.
Ifuatayo ni mlo kamili anaotakiwa apate mama mjamzito kila siku ya ujauzito wake kwa afya bora:

Maziwa na vyakula vya jamii ya maziwa: Glasi nne au zaidi ya maziwa ya aina yoyote pamoja na/au vyakula vyenye jamii ya maziwa kama jibini, mtindi,siagi, ice cream. Maziwa ni muhimu kwa protein, calcium, vitamins na virutubisho vingi. Vitasaidia ukuaji wa mifupa, misuli na nerves. Ni muhimu kwa damu yenye afya, kusaidia usingizi na kusawazisha mdundo wa moyo.

Mayai: Mayai mawili kwa siku husaidia kuupa mwili protein, vitamins minerals na vitamin A ambayo itasaidia kuzuia infections.

Protein: Serving mbili ya samaki, maini , kuku, nyama ya ngombe, mbuzi, kondoo au nguruwe, maharagwe au jibini. Kusaidia ujengaji mifupa, meno, misuli, ubongo na mwili kwa ujumla. Ukosekanaji wa protein ya kutosha kutasababisha kuchoka, uvimbe na kutojisikia kula au appetite ndogo.

Mboga za majani: Spinach, cabbage, collard greends, mchicha, matembele. Mboga hizi ziwe fresh na zile zenye rangi ya kijani iliyokolea(hizi ndio zenye virutubisho vya kutosha).  Mboga hizi zitakupa Vitamin A na B, pia virutubisho vitakavyosaidia mwili kuabsorb protein ya kutosha, ukuaji wa mwili, na utengenezaji wa damu. Kutopata mboga za kutosha kunaweza sababisha mama kupata anemia.

Whole Grains: Vipande vinne vya Mkate wa whole grain, mkate wa mahindi, vitaupa mwili vitamin B na carbohydrate kwa ukuaji wa misuli na nerves.

Vyakula vyenye vitamin C: Kipande kimoja au viwili vya machungwa au juisi ya ndimu, machungwa, nyanya. Vitamin C itasaidia uterus kuwa na nguvu ya kutosha ili kufanya kazi vizuri wakati wa labor, pia itasaidia kulinda mwili na infection na kusaidia kuabsorb iron kwenye mwili.

Siagi na mafuta: Serving tatu za maparachichi, siagi, olive oil au flax seed oil.

Matunda yenye rangi ya njano au orange: Huupa mwili vitamin A hii husaidia kulinda kibofu na figo kupata infections.

Maini kama unaypenda ni mazuri kwa protein pia.

Kunywa maji mengi ya kutosha. Maji huchangia kwa asilimia 75 ya uzito wa mtoto wako atakapozaliwa. Usipopata maji ya kutosha utaishiwa na nguvu kwa asilimia 20 na kupata matatizo ya dehydration na kichwa kuuma.
`
Chumvi ya kutosha kusaidia kuzunguka kwa damu kutoka mwilini kwenda kwenye placenta. Kutopata chumvi ya kutosha kunaweza kusababisha miguu kuuma na uchovu.

Kwenye sehemu ya pili tutaongelea virutubisho kadhaa na umuhimu wake kwa mama mjamzito na mtoto.

Thursday, March 1, 2012

Natural Birth Quote Of The Day - Birth is a Normal Process, not an ilness

No one actually thinks that childbearing is an illness, but many parents and childbirth professionals act as if it were. Make a place in your heart for normal birth. Release the myth of the laboring woman as some sort of invalid and replace it with an image of health and beauty. The laboring woman is radiantly healthy
"The Five essentials of a Positive, Healthy View Of Birth"
From Mind Over Labor By Carl Jones